Sunday, June 15, 2008

TAIFA STARS 0 - CAMEROON 0

Hapo juu ninaangalia mechi hiyo ya jumamosi
Mechi ya juzi kati ya Taifa Stars na Cameroon, niliishuhudia kama mdau wa soka wa Tanzania. Kwa ufupi sidhani kama Cameroon walicheza mchezo wao hasa na hawakuonesha sana kutaka kufunga kwa kila juhudi. Hali hii iliiweka timu yetu katika wakati mgumu lakini naamini kama watashambulia mechi ijayo basi Stars watapata nafasi ya kuwakamata na kuuwafunga.

Kama tutashinda mechi hiyo basi ndoto za kufuzu zitakuwa zimerejea japo kwa sasa mimi sina matumaini.

No comments: